Alhamisi, 2 Oktoba 2014

TAMBUA WEWE NI NANI?

TAMBUA WEWE NI NANI KTK ULIMWENGU WA  ROHO NA MWILI!
           Wakristo wengi siku hizi wanaishi bila kutambua haki na wajibu wao kwa Mungu, hii imeleta shida kwenye  wokovu wao hata wakaona kuwa wokovu ni mzigo. shetani naye amewapofusha macho wasije wakajua siri ya uwezo na ukuu walionao.Je wajua wewe ni nani?, Na una nafasi gani katika ulimwengu wa roho na mwili ? unajionaje? Wewe ni mshindi au umeshindwa? Je wewe ni dhaifu au mzima? Wewe ni masikini au tajiri? Neno linasema unavyojiona ndivyo utakavyokuwa- Mithali 23;7 unajitamkiaje? Unasema wewe u nani? Neno linasema mtu anakula matunda ya kinywa chake -Mithali 18;20,21 acha kukuri vibaya hata kama unajiona ni dhaifu sema mimi ni hodari Yoeli 3;10.Mara nyingine tunapotea kwa kutokuyajua maandiko wala uweza wa Mungu.Yesu akawajibu, “Mwapotoka kwa sababu hamjui maandiko wala uweza wa Mungu.Mathayo 22;29, Marko 12;24. Hebu tuone sala ya Paulo kwetu Efeso 1;18-23.Kumbuka kila neno lililoandikwa kwenye biblia ni kwa ajili yetu , Paulo anatuombea anasema;
        “Ninaomba kwamba macho ya mioyo yenu yatiwe nuru, mjue tumaini la mwito wake jinsi lilivyo: na utajiri wa utukufu wa urithi wake katika watakatifu jinsi ulivyo, na ubora wa ukuu wa uweza wake ndani yetu tuaminio jinsi ulivyo; kwa kadiri ya utendaji wa nguvu za uwezo wake: aliotenda katika Kristo alipomfufua katika wafu, akamweka mkono wake wa kuume katika ulimwengu wa roho; juu sana kuliko ufalme wote, na mamlaka, na nguvu, na usultani, na kila jina litajwalo, wala si ulimwenguni humu tu, bali katika ule ujao pia; akivitia vitu vyote chini ya miguu yake, akamweka awe kichwa juu ya vitu vyote kwa ajili ya kanisa; ambalo ndilo mwili wake, ukamilifu wake anayekamilika kwa vyote katika vyote.”
          Maneno haya yanatuambia kwamba Kristo alifufuka na kukalia kiti cha enzi cha Mungu., Je, wajua kwamba unatawala pamoja naye katika huo ulimwengu wa roho? Paulo anathibitisha jambo hili katika ufasaha kwenye maandiko mengine mawili: “akatufufua pamoja naye, katuketisha pamoja naye katika ulimwengu wa roho, katika Kristo Yesu” (Waefeso 2:6); “na ninyimmetimilika katika yeye aliye kichwa cha enzi yote na mamlaka(Wakolosai 2:10).
         Nataka nikukumbushe mambo ambayo bibilia imesema kutuhusu kuwa sisi ni nani? Kisha Yesu akawaambia wale Wayahudi waliomwamini, “Kama mkidumu katika maneno Yangu, mtakuwa wanafunzi wangu kweli kweli. Ndipo mtaijua kweli nayo kweli itawaweka huru.’’Yoh 8 31, 32. Hapo sina la kuongezea lakini naamini umejua kuwa kweli (neno) ikilijua linakuweka huru. Bwana Yesu asifiwe!.



MAMBO  YANAYOTUTAMBULISHA.

Ø WEWE NI UZAO MTEULE;.

Je unajua hilo “sema mimi ni uzao mteule” Kama mngekuwa wa ulimwengu, ulimwengu ungeliwapenda kama vile unavyowapenda walio wake. Kwa sababu ninyi si wa ulimwengu, lakini Mimi nimewachagua kutoka katika ulimwengu, hii ndiyo sababu ulimwengu unawachukia. Yoh 15;19
Si ninyi mlionichagua, bali Mimi ndiye niliyewachagua ninyi na kuwaweka mwende mkazae matunda na matunda yenu yapate kudumu, ili lo lote mtakalomwomba Baba katika Jina Langu, awape.Yoh 15;16
          Lakini ninyi ni taifa teule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu la Mungu, mlioitwa ili kutangaza sifa Zake Yeye aliyewaita kutoka gizani mkaingie katika nuru Yake ya ajabu. Mwanzo ninyi mlikuwa si taifa, lakini sasa ninyi ni taifa la Mungu. Mwanzo mlikuwa hamkupata rehema, lakini sansa mmepata rehema. 1pet 2;9.
Kwa maana alituokoa kutoka katika ufalme wa giza na kutuingiza katika ufalme wa Mwana Wake mpendwa, kol 1;13.

Kwa hiyo sisi tumehamishwa kutoka kwenye mambo ya dunia na kuingizwa katika ufalme au uraia mwingine ( katika ulimwengu war oho), japo bado tunaishi duniani lakini wenyeji wetu ni mbinguni, sawasawa na mtu anayeishi Malawi lakini ni mwenyeji wa Tanzania haimaanishi  yeye ni mmalawi. Kwahiyo usizifuate tabia za wamalawi yafikirini yaliyo juu siyo chini. Amen.
    Ikiwa umeokoka, tembea ukijua wewe ni tofauti na wengine na si lazima ufanye kila linalofanywa na wengine maana mengine si yanyoruhusiwa kwenye utaifa au uraia wako!, na kwa kufanya hivyo ulimwengu utakuchukia ,sisemi ujivune au ujibague  bali ujue kuwa kuna mambo ambayo watu wengine watafanya lakini wewe hutafanya maana una “speed governor” inayokuongoza na hii yamkini itasababisha ulimwengu kukuchukia! Take care, weka moja kichwani!!.

Ø WEWE NI MTAKATIFU;

“sema mimi ni mtakatifu’ mtakuwa watakatifu kama mimi nilivyo mtakatifu Lawi 19;2 mahali pengine anasema mtakuwa wakamilifu maana mimi ni mkamilifu pia biblia inasema katika zaburi- watakatifu waliopo duniani ndio ninao pendezwa nao.Pokea ahadi hiyo ni yako jua unayezungumziwa ni wewe mototo wa mungu usione hili neno aliyeandikiwa nimwingine, ni wewe mwenyewe. Kama unaamini kuwa una roho mtakatifu basi pia amini kuwa wewe ni mtakatifu kwa sababu roho mtakatifu hakai mahali palipo pachafu. Kwa habari ya Watakatifu walioko duniani, ndio walio wa fahari ambao ninapendezwa nao. Zab 16;3 kama wewe hutaki kujikubali kuna watu Mungu anawakubali na unavyo jiona ndivyo utakavyo kuwa kumbuka hilo pia. Kwa hiyo iweni wakamilifu kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu.’’Mathayo 5;48. Mpendwa umeshakombolewa na kusafishwa kwa damu yake ambayo haikumwagika bure bali ni kwa kututakasa . Katika Yeye tunao ukombozi kwa njia ya damu Yake, yaani, msamaha wa dhambi, sawasawa na wingi wa neema Yake Efeso1;7,4.
                                                                                 
Ø WEWE NI MWANA AU MTOTO WA MUNGU;

          Wewe si mtu wa Mungu bali u mwana! “sema nimefanyika kuwa mwana na nimehesabiwa haki”. Bali wote waliompokea, aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio Jina Lake. Hawa watoto wamezaliwa si kwa damu wala kwa mapenzi ya mwili au kwa mapenzi ya mtu, bali kwa mapenzi ya Mungu. Yoh 1;12
        Naamini na wewe unafanya hivyo yaani ulimpokea na unaamini,basi umefanyika kuwa mwana na kama ujuavyo mtoto wa kondoo ni kondoo, na mwana wa Mungu ni mungu mdogo!Roho mwenyewe hushuhudia pamoja na roho zetu ya kwamba sisi tu watoto wa Mungu.  Basi ikiwa sisi ni watoto, basi tu warithi, warithi wa Mungu, warithio pamoja na Kristo, naam, tukiteswa pamoja Naye tupate pia kutukuzwa pamoja .Rum 8;16 sisi warithi wa Mungu walithio pamoja na Kristo,kwa hiyo sisi sio watoto wa kambo kwa Mungu bali ni wana na ndio maana ni warithi pamoja na Kristo maana mtoto hana fursa ya kurithi.
 Kwa kuwa wote wanaoongozwa na Roho wa Mungu hao ndio watoto wa Mungu.Rum 8;14 Je wewe unaongozwa na roho? Kama ni jibu ni ndiyo-safi! maana wewe ni mwana wa Mungu.
       Kila mtu anayeamini kwamba Yesu ndiye Kristo amezaliwa na Mungu na ye yote ampendaye Baba humpenda pia mtoto aliyezaliwa naye.Hivi ndivyo tunavyojua kwamba tunawapenda watoto wa Mungu, kwa kumpenda Mungu na kuzitii amri Zake.Kwa kuwa huu ndio upendo wa Mungu, kwamba tuzitii amri Zake. Nazo amri Zake si nzito.Kwa maana kila aliyezaliwa na Mungu huushinda ulimwengu. Huku ndiko kuushinda kuushindako ulimwengu, yaani, hiyo imani yetu.Ni nani yule aushindaye ulimwengu? Ni yule aaminiye kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu.1yoh 5;1-4
           Oneni ni pendo kuu namna gani alilotupa Baba, kwamba sisi tuitwe watoto wa Mungu! Nasi ndivyo tulivyo. Sababu kwa nini ulimwengu haututambui, ni kwa kuwa haukumtambua Yeye. 1yoh 3;1
Ninyi ni rafiki Zangu mkifanya ninayowaamuru. Siwaiti ninyi watumishi tena, kwa sababu watumishi hawajui bwana wao analofanya, bali nimewaita ninyi rafiki, kwa maana nimewajulisha mambo yote niliyoyasikia kutoka kwa Baba Yangu.Yoh 15;14,15. Kwa hiyo kwetu Yesu ni Baba pia ni rafiki.
                                                                                                                            

Ø WE NI KUHANI NA MFALME ;

Sema mimi ni kuhani tena ni mfalme”unajua kazi ya kuhani namfalme? Najua unajua lakini makuhani enzi hizo ni watu ambao ndio tu waliokuwa wakirusiwa kuingia patakatifu lakini sasa nasi tumefanyika kuwa makuhani tunapaingia patakatifu kwa damu ya Yesu! Ufunuo 5;10 ,1;6 lakini kama ujuavyo mfalme ni mtu mwenye mamlaka, hatutegemei  mfame akiomba bali anaamuru Bwana Yesu asifiwe!.Wewe umewafanya hawa wawe ufalme na makuhani wa kumtumikia Mungu wetu,  nao watamiliki katika dunia.’’ Ninyi mtakuwa kwangu ufalme wa makuhani na taifa takatifu.’ Haya ndiyo maneno utakayosema kwa wana wa Israeli.  Kutoka19;6 . Nabii Isaya alikuwa ameona akasema, Nanyi mtaitwa makuhani wa BWANA,mtaitwa watumishi wa Mungu wetu.  Mtakula utajiri wa mataifa, nanyi katika utajiri wao mtajisifu.Isaya 61 ;6

Ø WEWE NI KIUMBE KIPYA;

 Ya kale yote  yamepita, iambie nafsi yako mimi ni kiumbe kipya! 2kor 5;17
Kwa hiyo kama mtu akiwa ndani ya Kristo, amekuwa kiumbe kipya, ya kale yamepita, tazama, yamekuwa mapya. Kwa hiyo kuwa huru kwa mambo yaliyopita usikumbuke Misri wala usitamani nyama za Misri hata kama kuna dhambi kubwa ulitenda jua Mungu haikumbuki maana amesema uovu wenu sitaukumbuka kamwe kwa hiyo hajui dhambi uliyotenda na anakushangaa. Anasema dhambi zenu zitakuwa nyeupe. Nimesulibiwa pamoja na Kristo, wala si mimi tena ninayeishi bali Kristo ndiye aishiye ndani yangu. Uhai nilio nao sasa katika mwili, ninaishi kwa imani ya Mwana wa Mungu, aliyenipenda na kujitoa kwa ajili yangu Gal 2;20.

Ø UMEBARIKIWA PAMOJA NA IBRAHIMU!

Sema hivyo ili ule matunda ya midomo yako Gal3;9 Kwa sababu hii, wale wote wanaoamini wanabarikiwa pamoja na Abrahamu, mtu wa imani. Hiii ni kwa sababu wewe unaamini kama Ibrahimu aliyekuwa akimwamini Mungu. Rum8;17 Basi ikiwa sisi ni watoto, basi tu warithi, warithi wa Mungu, warithio pamoja na Kristo, naam, tukiteswa pamoja Naye tupate pia kutukuzwa pamoja Naye.

Kwa hiyo, ahadi huja kwa njia ya imani, ili iwe ni kwa neema na itolewe kwa wazao wa Abrahamu, si kwa wale walio wa sheria peke yao bali pia kwa wale walio wa imani ya Abrahamu. Yeye ndiye baba yetu sisi sote. Rum 4;16 kwa hiyo lazima uamini na kuipokea ahadi hiyo ndipo itakuwa yako~maana anasema ahadi huja kwa njia ya Imani.
Kwa hiyo, wewe si mtumwa tena, bali ni mtoto, nawe ikiwa ni mtoto, basi wewe pia ni mrithi, mrithi wa Mungu. Gal 4;7


Ø UWEZO WA YESU NI UWEZO WAKO!

Sema nayaweza mambo yooote katika Yeye anitiayanguvu Fil 4;13
Nanyi ikiwa Roho wa Mungu aliyemfufua Yesu kutoka kwa wafu anakaa ndani yenu, Yeye aliyemfufua Kristo Yesu kutoka kwa wafu ataihuisha pia miili yenu ambayo hufa, kwa njia ya Roho Wake akaaye ndani yenu. .Rum 8;11 

 Yoh 14;12 Amin, amin, nawaambia, ye yote aniaminiye Mimi, kazi nizifanyazo yeye atazifanya, naam na kubwa kuliko hizi atazifanya, kwa sababu Mimi ninakwenda kwa Baba.Efeso 1;20 na uweza Wake mkuu usiolinganishwa kwa ajili yetu sisi tuaminio. Uweza huo unaofanya kazi ndani yetu, ni sawa na ile nguvu kuu mno Mungu alitufufua pamoja na Kristo na kutuketisha pamoja naye katika ulimwengu wa roho katika Kristo Yesu,Efeso 2;6

Ahimidiwe Mungu na Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo aliyetubariki sisi kwa baraka zote za rohoni, katika ulimwengu wa roho ndani ya Kristo. Efeso 1;3 hizi ni Baraka za rohoni ambazo ni kubwa kuliko zile za mwilini  ukiwa nazo hata kimwili umefanikiwa 3yoh 1;2 .13Tunajua kwamba twakaa ndani Yake na Yeye ndani yetu, kwa sababu ametupatia sisi sehemu ya Roho Wake. 1yoh 5;13

Ø WEWE UNA MAMLAKA;

“Nina mamlaka” Mathayo 16;19 Yesu akiisha kuwaita wale kumi na wawili pamoja, aliwapa mamalaka na uwezo wa kutoa pepo wachafu wote na kuponya magonjwa yote, kisha akawatuma waende wakahubiri Ufalme wa Mungu na kuponya wagonjwa. Luka 9;1
Kwa kuwa umempa mamlaka juu ya wote wenye mwili ili awape uzima wa milele wale uliompa. 3Nao Yoh 17;2
Tazama nimewapa mamlaka ya kukanyaga nyoka na ng’e na juu ya nguvu zote za adui, wala hakuna kitu cho chote kitakachowadhuru kwa namna yo yote.Luka 10;19

Ø WEWE NI MSHINDI;

Washindi Bwana Yesu asifiwe! Rum 6;14 1yoh 5;18 Yeye mwenyewe alizichukua dhambi zetu katika mwili wake, juu ya mti, ili kwamba,tukiwa wafu kwa mambo ya dhambi, tupate kuishi katika haki. Kwa kupigwa kwake, ninyi mmeponywa.1pet2;24
Nanyi ikiwa Roho wa Mungu aliyemfufua Yesu kutoka kwa wafu anakaa ndani yenu, Yeye aliyemfufua Kristo Yesu kutoka kwa wafu ataihuisha pia miili yenu ambayo hufa, kwa njia ya Roho Wake akaaye ndani yenu. Rum 8;11
Lakini ninyi, hamtawaliwi na mwili, bali na Roho, ikiwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu. Mtu ye yote ambaye hana Roho wa Kristo, yeye si wa Kristo. Lakini kama Kristo anakaa ndani yenu, miili yenu imekufa kwa sababu ya dhambi, lakini roho zenu zi hai kwa sababu ya haki.Rum 8;9 na kwasababu Yesu alishinda kwa habari ya dhambi na mauti nasi vivyo hivyo nasi ni washindi kwani tunamwamini mshindi nay eye yuko ndani yetu!

Ø WEWE UNA UUNGU NDANI YAKO;

 Rum 8;29 Nanyi ikiwa Roho wa Mungu aliyemfufua Yesu kutoka kwa wafu anakaa ndani yenu, Yeye aliyemfufua Kristo Yesu kutoka kwa wafu ataihuisha pia miili yenu ambayo hufa, kwa njia ya Roho Wake akaaye ndani yenu. Rum 8;11 roho wa Mungu anakaa ndani yetu.
Uweza Wake wa uungu umetupatia mambo yote tunayohitaji kwa ajili ya uzima na uchaji wa Mungu, kwa kumjua Yeye aliyetuita kwa utukufu Wake na wema Wake mwenyewe 2pet 1;3 Kisha BWANA akamwambia Mose, “Tazama, nimekufanya kuwa kama Mungu kwa Farao, naye Aroni, huyo ndugu yako, atakuwa nabii wako. Kutoka 7;1

Ø WEWE NI NURU NA CHUMVI PIA;

Mathayo 5;14 Ninyi ni nuru ya ulimwengu.
 Yoh 8;12Kwa maana zamani ninyi mlikuwa giza, lakini sasa ninyi ni nuru katika Bwana. Enendeni kama watoto wa nuru (kwa kuwa tunda la nuru hupatikana katika wema wote, haki na kweli,) nanyi tafuteni yale yanayompendeza Bwana. Msishiriki matendo ya giza yasiyofaa, bali yafichueni.  Efeso 5;8-11. ‘‘Ninyi ni chumvi ya ulimwengu. Lakini chumvi ikipoteza ladha yake, yawezaje kurudishiwa ladha yake tena ? Haifai tena kwa kitu cho chote, ila kutupwa nje ikanyagwe na watu. Math 5;13

Ø WEWE NI TAJIRI;

2kor 8;9 Kwa maana mnajua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, kwamba ingawa alikuwa tajiri, kwa ajili yenu alikubali kuwa maskini, ili kwa umaskini Wake ninyi mpate kuwa matajiri.
 kol 1;13 1yoh 4;43 Ikiwa Mungu hakumhurumia Mwanawe, bali alimtoa kwa ajili yetu sote, atakosaje basi kutupatia vitu vyote kwa ukarimu pamoja Naye? Rum 8;32 Hivyo basi, mtu asijivune kuhusu wanadamu! Kwa kuwa vitu vyote ni vyenu, ikiwa ni Paulo au Apolo au Kefa au dunia au uzima au mauti, au wakati uliopo au wakati ujao, haya yote ni yenu na ninyi ni wa Kristo, naye Kristo ni wa Mungu. 1kor 3;21-23

                                                      
Ø WEWE NI HEKALU,KIUNGO NA TAWI;

Je, hamjui ya kwamba ninyi ni hekalu la Mungu na kwamba Roho wa Mungu anakaa ndani yenu? Kama mtu ye yote akiliharibu hekalu la Mungu, Mungu atamwangamiza mtu huyo, Kwa maana hekalu la Mungu ni takatifu,
ambalo ndilo ninyi.1kor 3;16 Je, hamjui kwamba miili yenu ni viungo vya Kristo? 1kor 6;15. Miili yetu ni hekalu na si hekalu letu sisi bali ni la roho mtakatifu na tumeazimwa tu, bali tuifanyie kazi vizuri ili mmiliki (roho mtakatifu) afurahi siku zote!.Mahali pengine anasema mimi ni mzabibu nanyi ni matawi.

                                           
Ø WEWE NI RUNGU LA BWANA LA VITA;

Mungu anasema kuwa wewe ni Silaha yangu ya vita  kwa wewe navunjavunja mataifa,kwa wewe naangamiza falme, kwa wewe navunjavunja farasi na mpanda farasi, kwa wewe navunjavunja gari la vita na mwendeshaji wake, kwa wewe napondaponda mwanaume na mwanamke,  kwa wewe napondaponda mzee na kijana,  kwa wewe napondaponda kijana wa kiume  na mwanamwali,  kwa wewe nampondaponda mchungaji na  kundi, kwa wewe nampondaponda mkulima na maksai, kwa wewe nawapondaponda watawala na maafisa. “Mbele ya macho yako nitamlipiza Babeli na wote waishio Ukaldayo kwa ajili ya makosa yote waliyofanya katika Sayuni,’’ asema BWANA.Yer 51;20-24



v KUKIRI

Baba Mungu mfalme wa wafalme uketie mahali pa juu palipo inuka sana, asante kwa neno lako lililonifikia leo ili kunijulisha na kunikumbusha nafasi yangu ! Neno lako linasema nitakula matunda ya midomo yangu nami najitamkia na najitambua kuwa mimi ni uzao mteule,mimi ni mtakatifu, mimi ni tajiri,mimi ni mzima,mimi ni mshindi,mimi ni rungu lako Bwana,mimi ni chumvi na Nuru ya kuwaangazia wengine,mimi ni mshindi na nina mamlaka, mimi ni kuhani na mfalme katika jina la Yesu Kristo Mungu nisaidie kutembea na kujua mimi ni nani na nafasi yangu niitumie ipasavyo katika Jina la Yesu kristo nimeomba. Amen!

HAYA NI BAADHI TU YA MAMBO MENGI TULIYOANDIKIWA KWENYE BIBLIA~ILI KUELEWA ZAIDI MAMBO HAYA NA NAFASI YAKO NAKUSHAURI UANZE KWA KUSOMA  KITABU CHA WAEFESO HUKU UKIMWOMBA ROHO MTAKATIFU  AKUSAIDIE  ZAIDI ILI UPATE KUELEWA! MUNGU AKUONGOZE NA AKUBARIKI SANA! AMEN!
Lakini mambo haya Mungu ametufunulia kwa njia ya Roho Wake. Roho huchunguza kila kitu, hata mambo ya ndani sana ya Mungu 1kor 2;10











                                                                                                                                        
ü 0756688789

ü SEME FREDY .A.

 

Maoni 1 :