Jumatano, 24 Desemba 2014

   UMUHIMU WA KUMSHUKURU MUNGU KWA KILA JAMBO;   EFESO 5;20.
     
                Namshukuru Mungu kwa kutufikisha mpaka siku na  masaa machache yamwaka huu(2014) zimebaki siku saba(7) tu sawa sawa na masaa (168 )mia moja na arobaini na nane ,ili tuumalize mwaka huu(2014) na tuingie mwaka 2015, hii ni neema,haleluya!.Ukitaka uishi kwa furaha na amani  na upate sababu zaidi za kumshukuru Mungu,tafakari yale tu Mungu aliyokutendea wewe kwanza wala usijilinganishe na mwingine kwa maana kila mtu Mungu ameipanga ratiba au plani  ya masha yake .
               Leo nataka tukumbushane umuhimu wa kumshukuru Mungu kwa kila jambo.kila mtu kuna vitu ambavyo amepitia vinaweza vikawa vizuri au vibaya au vyote kwa pamoja lakini sababu ya kumshukuru Mungu ipo kwa hali hizo zote haijalishi. Mungu anasema “Atoaye dhabihu za shukrani ananiheshimu mimi, naye aiandaaye njia yake jinsi ipasavyo nitamwonyesha wokovu wa Mungu.’’(zaburi 50;23).Tumshuru Mungu na maandalio ya mioyo yetu yawe katika mtazamo wa kumtegemea Mungu kwa mwaka  mwaka ujao.

            Tunapaswa kumshukuru na kumtukuza Mungu kwa kila jambo liwe lenye furaha au amani. Maana huwezi ukajua unachoona ni kibaya kumbe kwa Mungu ni kizuri na ana mipango mizuri na wewe! Huwezi ukajua kuwa mungu amekupigania kwa kiwango gani au namna gani, na badala ya kutokia hicho kilichotokea  pengine kingitokea kibaya zaidi ya hicho.kwahiyo tunachopaswa ni kushukuru  na kumsifu mungu hajalishi umepitia katika mambo  mazito na magumu kiasi gani lakini mungu alikuwa na plan ana mpango na maisha yako kwahiyo si vabaya ukamshukuru Mungu kwa namna zozote unaoona zinafaa.. Paulo anasema “sikuzote mkimshukuru Mungu Baba katika Jina la Bwana wetu Yesu Kristo kwa kila jambo.(Efeso 5;20)
       Mimi nimejifunza kumshukuru Mungu na kumtukuza Mungu hata kwenye wakati mgumu na katika mambo yanayoudhi na kusikitisha na haya niliamua kuyweka kwenye matendo, yaani kila nilipo pata kitu  Mungu alinikumbusha kumwambia asante, nikifanya hivyo napata amani  na ndipo nilijua hakika Mungu anatupenda sana haijalishi ni  mambo gani tunayopitia.kwa kifupi unapomshukuru mungu kwa kila jambo unapata yafuatayo;
       I.            Amani ; unapoenda mbele za Mungu na kusema “Mungu nakushukuru kwa yote na ninakutukuza”   unapata amani kwa maana umesalenda kwa Mungu na huo mzigo uliokuwa nao unakuwa umemtwika Mungu(1peto 5;6). Mfano umepata hasara ya mradi wako unapomshukuru Mungu na kumtukuza kwa moyo wako wote unapata amani maana pia  unakuwa umejinyenyekeza hata kama ulikuwa na uchungu uanaisha unapata amni ya Kristo. Liweke hili  katika matendo hili ili ujue nini namaanisha.
    II.            Unapata majibu; mungu anaweza kukuambia kuwa mwanangu nimeliruhusu hili litokee au likupate kwa sababu……..kwa hiyo bado unakuwa ujua kinachoendelea ktk maisha yako na hii itakupa ujasiri. Lakini usipopata muda wa kushukuru huwezi ukajua chochote zaidi utaumia,utachanyikiwa na mbaya zaidi utaanza kulalamika.
 III.            Mungu anajivunia wewe  maana hata katika shida pia kuna sifa mbele za Mungu ni kama Paulo na sila gerezani (Matendo 16;25), sifa zao kwa Mungu hazikuzima,ni kama ayubu hakuacha kumshukuru Mungu pamoja na shida zake.Sasa hapo shetani anasema huyu simwezi tena maana nilijua hapa ndipo atakapo tamaa lakini ndo sifa zake zimekuwa za juu mbele za Mungu wake. Na mungu anatabasamu anasema  hakika mwanangu amenijua.
IV.            Kiwango chako cha imani kinapanda; kadri unapopitia magumu na majaribu  ya kuvunja moyo, ndipo imani yako huongezeka. Pia hiyo ni gia ya kusonga mbele maana  ukishinda unarudia ukiweza unasonga mbele zaidi (Yakobo 1;2-3 Ndugu zangu, hesabuni kuwa ni furaha tupu mnapopatwa na majaribu mbalimbali, kwa sababu mnajua ya kuwa kujaribiwa kwa imani yenu huleta saburi.
   V.            Unapomshukuru na kumsifu Mungu wakati wa shida unavuka eneo la kulalamika na ambalo ni baya sana maana najua  unakumbuka kilichowapata wanawa Esraeli walipokuwa wakilalamika.

Haya ni baadhi tu ya mengi lakini tumuombe Mungu atupe moyo wala shukurani atuepushe na kulalamika.

 Ningipenda kusema pia kuwa ;usithubutu kumuacha Mungu kwa chochote au kwa lolote bali acho chochote au lolote kwa ajili ya Bwana
Anza na Bwana;maliza na Bwana anayeanza na kumaliza  na Bwana hufanya  vema sana  nakutakia mwisho mwema wa mwaka 2014 na mwanzo mwema wa mwaka 2015, kwa kila jambo utakalo lifanya mwaka 2015, Mungu akatangulie mbele yako, liliogumu likawe jepesi katika jina la Yesu uliposhindwa mwaka 2014, mwaka 2015 ukashinde nakutangazaia ushindi wako kwa mwaka 2015 katika jina la Yesu. Mungu akahusike na siku zote 366(mia tatu sitini na sita) zilizoko ndani ya mwaka!, miezi yote 12( kumi na mbili ) ya mwaka ,wiki zote za mwaka siku zote za mwaka ,masaa, dakika na hali kadhalika sekunde. Mungu akawe pamoja nawe na Roho wake akakuongoze katika Jina la Yesu Kristo jina lenye nguvu lipitalo majina yote ameni.!


Nakutakia heri ya Krisimasi na mwaka Mpya. Wewe umebarikiwa!